Sunday, 12 July 2020

Maisha Baada Ya Chuo

maisha baada chuo
Wasomi wengi sana especially ambao bado wapo mashuleni huwa wanafikiria kuwa watasoma mpaka shule ya msingi,sekondari,sekondari ya juu na chuo baada ya chuo wataajiriawa nakufanya kazi na kupokea mshahara alafu watajenga nyumba na kuwa na maisha mazuri. 
  • Mfumo wa elimu Tanzania unaanda wasomi waje kuwa waajiriwa na sio kujiajiri mwenyewe wala kujitegemea kwa kipato.
Sasa maisha baada ya chuo kwa wasomi wote huwa yanakuwa hivi
  • Kuna wale ambao watakuwa wanajitolea na hawalipwi kabisa
  • Kunaambao watakuwa wanajitolea na kulipwa kidogo, inafika wakati wanaona mda unakwenda na hakuna connection zozote zile mwishowe wanaacha
  • Kuna ambao watakwenda kufanya biashara mtaani(best of all) 
  • Kuna ambao watakuw wapo nyumbani tu hawana hili wala lile wanaangalia degree zao na kuchagua kazi maana wanaona hawana hadhi ya kufanya kazi ambazo sio za kisomi(worst kind) 
  • Kuna ambao watapata ajira katika sekta binafsi lakini wanaona kipato hakikidhi mahitaji
  • Kuna ambao watakuja kuwa wadangaji kwasababu ya ugumu wa maisha
  • Kuna ambao watakuwa wanapiga mishe za hapa na pale ili kupata hela za kuishi(mishen town) 
  • Kuna ambao watakuwa wakulima
  • Kuna ambao watakuwa wafugaji
  • Kuna ambao watakuwa inspiration talkers reality they got nothing 
  • Kuna ambao watakuwa wanabeti tu na kukwambia ramani hazisomi
  • Kuna ambao watakwenda kusoma masters
  • Kuna ambao watakuwa wanasiasa tu kwasababu wanatafuta pakutokea
  • Kuna ambao wataamua kuwekeza kwenye haya makampuni kama global alliance, forever living c, oriflame, na mengineyo mengi mpaka waje kusanuka kuwa huo mfumo hauwafaidishi wao ila walio tangulia kabla ndio wanaopata faida 
  • Kunaambao watakuwa wanajaribu kupata mafanikio the hard way(strugglers) ambao siku zote huwa watafanikiwa 
  • Kunaambao watakuwa wanajaribu hili na lile lakini huwa wanakata tamaa mapema na kushindwa kufikia lengo.
  • Huwa kuna aina nying sana za maisha na watu ambao watatokea baada ya masomo na baada ya kuanza maisha ya uraiani.
  1. News flash kwa wasomi wote kwamba the struggle is real especially to those ambao mnasoma bado muwe na mind set kwamba nikimaliza masomo sio lazima niajiriwe buni mbinj za kujipatia kipato ili uweze kuwa na maisha mazuri huko mbeleni, uwe umesoma ama haujasoma biashara au kazi yeyote ile hufanywa na watu wote hainaga kiwango cha elimu sema tofauti utaionyesha wewe ambae umesoma kwa kuifanya kazi yako kisomo na kwa uweledi wa juu kabisa onyesha elimu yako inakusaidi vipi kufanya biashara ama kazi uliyochagua kuifanya kwa quality ya juu kiasi gani ili iwe tofauti na ya watu wengine. 
  2. Think critically kama kwel wataka kutoka kimaisha jiwekee goals au target ya kwamba baada ya mwaka au miaka mingapi wataka kuwa na mafanikio kiasi gani, wataka kuwa na maisha ya aina gani ila sio kulala na kuwaza hela mwishowe uje kupata depression bure wakati haujishughulishi
  3. Kuwa na role model ambae utakuwa unalook up to him and desire to be economically better than him or at least reach where he is and more.
Siku zote huwa nasema if you want to be remembered with the future generations leave the greatest legacy behind you will never be forgotten.
BE THE LEGEND. 


Wednesday, 8 July 2020

UZEMBE wa MADAKTARI NA MANESI

uzembe wa madaktari na manesi katika kazi zao
Siku zote tunaamini madaktari sana, sasa uzembe mdogo wanaofanya madaktari na manesi unaweza ukapoteza maisha ya watu.Sisemi Vibaya ni bora Kuchukua tahadhari kuliko kuliko kujutia baadae.

Kuna mtu alikuwa anaumwa, kupelekwa hospital bila hata kujua historia ya mgonjwa vizuri wakamweka karantini,mtu anaumwa yupo serious kabisa lakini they overlooked kila kitu na kuhisi ni Corona, mgonjwa anahistoria ya kuumwa kifua, kama miaka mitatu sasa huwa anasumbuliwa na pneumonia, anatatizo la kutanuka, hakuwa na mafuwa wala kikohozi, joto la kawaida, alafu unampatia dawa za kutibu dalili za corona to be exact walikuwa wanampatia Azithromycin 250mg 2*2 kwa siku, mpaka akaanza kuzitapika yaan akimeza tu dawa anazirudisha that's how her body was protecting itself, overlooking details when it comes to health issues can be lethal.

Kuumua mtu mwenye pumu hauhitaji kumchoma sindano ya sumu, mtu akibanwa na kifua hawezi kupumua vizuri, unahis kama vile pumzi inataka kukata kabisa, ndio dawa ni muhimu maana inasaidia ila huwe safi ni muhimu sana maana ukikosa hewa safi mtiti ni ule ule, kumweka mtoto mdogo ambae amebanwa na kifua kwenye chumba ambacho kinanuka chlorine unategemea nini? Kinachoshangaza zaidi ni kuwa mtoto mdogo possibly <2 year suspected kuwa na corona wakati wazazi wake hawana, mtu mwenye pumu anaweza kuwa treated na dawa tofauti tofauti depends with how chronic ur illness is, no perfume,sprays,dust,stong scented oil and no cold, literally ur living a life of avoiding any strong smells and dust as much as you can so definitely no chlorine smell, i don't know who should be blamed for the death of that kid.

Mgonjwa ameletwa hospital yupo serious amelala kwa kitanda alafu hapati msaada wa haraka anaachwa OPD mpaka inafika wakati nduguzo wana mwinua mkono na kuuachia kuona kama bado yupo mzima, kwa hali kama hiyo alafu mbele za wagonjwa wengine kila mtu anapanic kivyake kila mtu anaona sasa ukisikia kifo kimekaribia ndio leo alafu bado we have to trust doctors and nurses.

Some doctors are always drunk na ndio amekuja kazini what can you say and ur sick you got no option just praying to God hoping he is not drunk enough to prescribe anything that comes to his mind.

Sometimes we have to question everything kujua kipi ni sahihi na kipi sio sahihi, don't trust blindly its lethal.


Thursday, 2 July 2020

JPM ANAFAA KWELI 2020 ?

jpm anafaa kwel 2020?Mtashangaa sana kwanini nasema kuwa 2015 uchaguzi ulifanyika na 2020 unafanyika tena.

Maana yangu kubwa ni kwamba utaona watu wengi sana wanasifia wanasiasa jambo ambalo sio baya ila watanzania tunatakiwa tuwaze sana ili tusije tukafanya mazoea kama tunavyofanya kila mwaka wa uchaguzi ukifika, hakuna sheria inayosema kwamba ni lazima kiongozi akae miaka kumi madarakani kama anafaa mpatieni dola aendeleze gurudumu lake la maendelea na kama hajatenda kama apaswavyo piga chini chagueni mwenye lengo jema la kuleta maendeleo.

1. Madiwani
..Jiulizeni sana diwani aliekuwepo madarakani amewatendea jambo gani la maendeleo katika kata zenu?
..diwani ametoa wazo gani katika kuleta maendeleo katika kata anayoitumikia?
..je diwani huyo mkimchagua tena atawaletea jambo gani katika kata yenu

Ni jukumu lenu kama wananchi kuchagua kiongozi bora ila mabadiliko na maendeleo ya patikane katika jamii yenu.

2. Wabunge
..mbunge wa wilaya yako amekuletea jambo gani la maendeleo kwa miaka mitano aliyokuwa madarakani?
Unfortunately mbunge wa wilaya niliyopo mimi yeye alichokifanya ndani ya miaka mitano ni kununua gari lake tu, hakai ofisini wala hoja zake zote alizotoa sidhani kama amezitimiza.
..je mbunge wako alitimiza ahadi zake alizotoa wakati wa kampeni miaka mitano iliyopita?
..je atafaa tena kuwepo madara kani?

3.Raisi
..raisi aliepo madarakani ametimiza hoja zake alizoto/ahidi wananchi?
..je ameleta maendeleo gani katika miaka mitano aliekuwepo madarakani?
.. Changamoto ya umasikini kwa mtu mmoja mmoja ameitatua vipi? Tena angalieni sana watu ambao wapo mijini na vijijini ambao wapo kwenye mzunguko wa umasikini usiangalie wale watu ambao ni matajiri ndio mtajua ninachokimaanisha ninauhakika kuna yule mtu apo mtaani kwako ambae unamuonea hafi huruma maana hata chakula cha siku hajui atakipataje na hajui hata kama kesho ataamka, anakula mlo mmoja siku nzima, nguo ndo bas tena kesho ikifika ni majaaliwa mateso yale yale ya jana tena bora na jana yake, masikini wamesaidika vip?
..Aliyotenda yanaonekana na ambayo hayajatendeka yanaonekana je ametenda kwa asilimia ngapi?
..kutokana na asilimia ulizo mpa je anafaa kuwa madarakani tena?

Watanzania tuko na tatizo moja tu yaan utazani tuanaugonjwa wa kusahau, msikubali kuhongwa vijihela vya mboga ya kula jioni tu alafu ukajitia hasara na kupoteza miaka mitano ambayo ungepata mafanikio na kupata pesa za kutumia miaka yote hiyo mitano na kwa siku nzima, tusikubali kuchagua mtu ambae hatatuletea badiliko lolote katika miaka mi tano ambayo unampa akaipoteza bure, tusikubali kugongwa kama mpira wa kona na kuingia nyavuni wakati ungekuwa unafutahia kuwa uwanjani unawapa wachezaji changamoto.

Tuondoe dhana kuwa kiongozi ni yule anaetoka chama fulani, hapana, kiongozi bora anatoka chama chochote, kiongozi mwenye sera na uchu wa maendeleo katika wilaya, kata, mtaa, na hata nchi yake huyo ndio kiongozi anaetufaa, kiongozi ambae anakuwa sauti ya kwel ya wananchi ndio anaefaa, kiongozi ambae akikaa hata katika familia yake anatamani na anakuja na wazo jipya ya kuiimarisha familia yake kiuchumi ndio anaefaa, kiongozi ambae anaona baada ya miaka mitano jamii yake ataibadilisha katika nyanja mbali mbali ndio anaefaa.

Mwaka wa uchaguzi tufanye maamuzi sahihi bila kushurutisha na nguvu ya vijihela vya chini ya kapeti wala nyuma ya pazia, tufanye maamuzi sahihi kwaajili ya baadae sio kwaajili ya sasa tu ata wajukuu zenu waje kuwakumbuka kwa kufanya jambo zuri huko baadae.

If you want to be a legend leave a great legacy behind no one will forget you forever.