Tuesday, 28 March 2023

*MHE. KIKWETE AELEKEZA WARATIBU WA TASAF KATIKA HALMASHAURI KUPATIWA ELIMU YA KUWAHUDUMIA WALENGWA KWA UPENDO.*

Lengo la kuanzishwa kwa TASAF ni kuwawezesha watu wasiojiweza kabisa kiuchumi kuondokana na hali iyo duni kuwapa ruzuku itakayowasaidia kupiga hatua ya maendeleo kiuchumi, hivyo ni vyema waratibu wakapewa ujuzi ya namna ya kuwahudumia walengwa hao.


Mh Kikwete ametoa maelekezo hayo jijini Dar Es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa TASAF.


Mh Kikwete amesema "Lengo la kuanzishwa kwa TASAF ni kuwawezesha watu wasiojiweza kabisa kiuchumi kuondokana na hali iyo duni kuwapa ruzuku itakayowasaidia kupiga hatua ya maendeleo kiuchumi, hivyo ni vyema waratibu wakapewa ujuzi ya namna ya kuwahudumia walengwa hao".


Kuna changamoto kubwa kwa baadhi ya waratibu wa TASAF katika Halmashauri kutowahudumia vizuri walengwa wa TASAF, ni vema wakapewa elimu ya kuweza kuzungumza na walengwa kwani fedha zimetengwa kwaajili yao, wasipohudumiwa kwa upendo itakua haina mana ya kuanzishwa kwa mfuko huo.


Mh Kikwete amesema "Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Dkt Samia Suluhu anatamani kuona wananchi wote wanainuka kiuchumi, hivyo walengwa wakihudumiwa kwa upendo na kuelekezwa namna ya kutumia ruzuku basi malengo ya Mh Rais yatakua yamefikiwa".


Aidha Mh Kikwete ameitaka Menejimenti hiyo kupitia kitengo cha habari kuuhabarisha umma juu ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi yao ioi kuepusha watu wasio na nia njema kuzungumza mabaya juu ya utekelezwaji wa majukumu ya TASAF.


Mh Kikwete amesema "TASAF inafanya kazi nzuri ya kuwainua walengwa kiuchumi, lakini mazuri hayo hayasemwi mara kwa mara, hivyo ni vizuri yakasemwa ili kuepukaba na watu wanaoharibu taswira nzuri ya taasisi na serikali kwa ujumla.

Saturday, 25 March 2023

HOW TO START A SUCCESSFUL BUSINESS THAT BRINGS PROFIT/ JINSI YA KUANZISHA BIASHARA INAYOINGIZA FAIDA.

Leo nataka niwaambie kitu kuhusu biashara, namaanisha jinsi ya kuifanya biashara yako ikuingizie faida na sio hasara , hapa ndipo mahali watu wengi hufeli. Sintakwambia sijui tengeneza mpango kazi fanya expected profit or loss / faida au hasara utakayo ipata kwa week au mwezi , Vitu muhimu vya kufahamu kwa wewe mfanya biashara au unategemea kuanzisha biashara yako.ndio mpango kazi ni mihimu tena muhimu sana ila kuna vitu vikikosekana hata kama unampango kazi mzuri basi biashara yako itafeli

Vitu muhimu vya kufahamu kwa wewe mfanya biashara au unategemea kuanzisha biashara yako.
1.commitment /kujitoa au kujitolea au kuwekeza muda wako katika kuijenga biashara yako, usipo weka muda wako katika biashara yako my friend iyo biashara itakufa kabla hujaianza.
2.kuthubutu usiogope kujaribu njia mpya za kukuza biashara yako jifunze kwa wale ambao tayar walisha kuwa wanafanya biashara na ujiongeze na usiogope kujaribu jambo jipya maana usipo jaribu hutaweza kujua kama kingefabya kazi au la.
3. Be innovative/ kuwa mbunifu katika biashara lazima uwe mbunifu sio sababu jiran yako anapika maandazi bas na ww upike maandazi swali ni je hayo maandazi yako yanautofauti gani na ya wengine yaani ni kitu gani kinakufanya uwe watofauti na kushawishi mteja arudi  na kesho tena??
4. Kauli, unaweza ukawa na vitu vizur lakini hupati mteja tatizo ni kauli yako unaweza ukawa na kauli chafu au huongei na wateja basi huwezi pata wateja mteja ndio bosi wako au mfalme wako kwaiyo akija mchangamkie mkaribishe kwa bashaha muulize ahitaji kitu gani mwonyeshe vitu tofauti tofauti mweleze na vitu vingine vilivyopo uone kama kesho hajarudi tena na atakuletea pia wateja wengine kutokana na kauli yako
5. Matumizi, usifanye matumizi au usitegemee biashara yako kwa kila kitu namaanisha unaanzisha biashara bado haijawa imara halafu unategemea pesa za matumizi yako binafsi kutoka kwenye biashara hiyo, biashara zote mwanzoni zinakula pesa badala ya kuingiza kwaiyo ukifanya kuitegemea kwa kila jambo biashara hiyo itafeli
6.kitahidi kuwa na miradi inayokuingizia pesa, usitegemee mradi mmoja ambao unakuingizia pesa  ndo ukawa kila kitu jiwekeze katika vitu tofauti tofauti uwe na vyanzo tofauti tofauti vya kukuingizia pesa hutojutia utakuja nishikuru baadae sababu kubwa ni kwamba kuna risk ambazo watu huwa hawazifikirii ambazo zinawezq kusababisha biashara yako ikapotea au kufa ukiwa na vyanzo vingi basi utaweza kujikimu vizur pia
7.management, sio kila mtu anaweza kaa katika biashara yake mwenyewe kwaiyo kama umeweka mtu basi hakikisha huyo mtu ni mwaminifu na anajua kufanya biashara namaanisha uwe umemchunguza mfanya kazi wako na kujua uwezo wake wa kikazi na umeridhika na kiwango chake cha kazi ndio umwache mwenyewe lakini pia hakikisha unakwenda kumtembelea katika biashara mara kwa mara ili kujua biashara inaendelea vipi.

Kama wahitaji kujua kuhusu mpango kazi/ business plan unaweza ukajifunza hili katika post yangu ambayo tayar nilisha itoa kwaiyo darsa huru unalipata hapa ukiwa na jambo la kuuliza usisiste  pia unaweza nipata kwa email happyissangya1@gmail.com na pia unaweza jiunga goup la whatsapp via https://chat.whatsapp.com/HVhM857PCIu4oemMIoAasu