Thursday, 11 January 2024

SIASA BHANA WACHA ZIWE HADITHI

​Unaambiwa United Republic Of Tanzania ni democratic nations ila bhana hiyo demokrasia iko wapiii???

Wanasisa njoeni mnichape kama nimesema uwongo,

1. Ahadi zile zile ambazo hazitimizwi

mtaani kwetu sijui mbunge yupo wapi??

2. Gharama ya maisha ndio inazidi kuwa ghali kila leo ila resources Tanzania inamiliki inatosha kwa Tanzania kuwa taji

3. Mikopo ya nje inazidi kuongezea ila project ambazo zinakamilishwa haziendani na fungu lililopekelewa kutoka pahali mmekopa.

4. Pesa ambazo zipo allocated kwaajili ya project fulani hazifiki kwa wakati katika maeneo husika na pia hakifiki kiasi halisi ambazo zilipangwa namaanisha hapo kati wamezipiga juu kwa juu.

5. Baada ya kupata kura hata kuongea na wananchi wako walio kupa fursa ili kuwasaidi hutaki ama ndo tuseme mnafunga tinted zenu.

6. Project nyingi ambazo zimekamilika zipo chini ya kiwango na mnafungia macho tu ila sababu mnaifahamu na watanzania wanafahamu pia ila kusema sasa ndio tatizo.

7. Kukosoa serikali ni kama jambo ambalo haliruhisiwi alafu bado mnasema eti Tanzania ni nchi huru.

8. Taasisi kama ya MAHAKAMA, TUME YA KUSIMAMIA UCHAGUZI na PCCB zipo chini ya serikali unategemea wanaweza kufanya kazi zao effectively bila kuwa waza mwajiri wake atamwondoa kazini bila kufikiria mara mbili.

Cha ajabu pahali panapoongoza kwa rushwa ni MAHAKAMA.

9. 2024 ni mwaka ambao vitu vingi vitafanywa kwa kulegezwa fulani ili kupata kura kirahisi.

10. 2024 ni mwaka ambao wasema ukweli wengi watapotezwa sana


Tukiwa wa kweli watanzania mnahongwa majiko madogo ya gesi, vitenge sijui khanga, tsheti na vielfu kumi hakafu unampa dhamana mtu ambae baadae anakuwa hana msaada kwako.

Natamani kucheka kama mazuri vile ila inasikitisha sana kama bado tutaendelea kufanya makosa yale yale kila baada ya miaka mitano kwa kujirudia rudia, najua ideology’s huwa zinatofautiana ila kutumia hata ule msemo wa MWAMBA NGOZI HUVUTIA KWAKE naona kama vile tunashindwa, wakati wa kuchagua usiangalie mtu anakupa nini kwa wakati ule ila angalia anauwezo wa kukupatia nini kwa baadae na kama kinafaida zaidi au la?. 

DARASA HURU “UKIPEWA POKEA ILA AKILI KICHWANI KWAKO ANGALIA FAIDA YAKO YA BAADAE”.

ANZA NA ULICHONACHO

​Mtaji wa masikini bwana ni nguvu zake kwaiyo anza na ulicho nacho embu fanya 2024 kuwa mwaka wa mabadiliko katika maisha yako.




Kwenye maisha tupo na hali tofauti za kiuchumi, kuna waliozaliwa wako na bahati kwao wako na pesa angalau anaweza kupewa mtaji ila ni vizuri kuwa na kile kitu unaweza sema kwa pride kwamba nichako na umekipambania mwenyewe.

Kuna ambao wao mtaji wao ni nguvu sasa panahitajika uvumilivu na mipango ili kupata kile unataka na kuwa na maisha ya aina fulani unayoyataka kuyaishi.


Nikisemema mataji wako ni nguvu zako na pia anza na kile ulichonacho namaanisha tengeneza plan/ mpangilio wa jambo unalotaka kulifanya na pia utengeneze picha kwenye akili yako kwenye miaka mitano ijayo unataka kuwa nani??


Mfano unafanya kazi unalipwa pesa ila sasa hakikisha kuna asilimia ya pesa hiyo unaiweka ili angalau jambo lako unalotaka kulikamilisha ulifanye.


Fact ni lazima kutumia pesa kutengeneza pesa ila kwenye matumizi ya pesa sasa ndio unaweza ukatumia pesa ndogo kuanzisha jambo lako na uzuri wa biashara ni kuwa biashara inakuwa kutokana na asilimia ya faida unakuwa unairudisha kwenye biashara yako.


Fact usitegemee kuona mafanikio kwa muda mfupi lazima kukuza jambo lako kwanza ndio utakapoona faida yake kwaiyo uvumilivu na ubunifu ni jambo la lazima.


Fact usitegemee kila hitaji lako katika jambo lako unalolifanya especially kama ni biashara utaishia kula mtaji wako.


Fact usiweke mayai yako yote katika kapu moja, jaribu kuwa na sehemu tofauti tofauti au biashara mbali mbali ambazo zinakuingizia maokoto


Fact simamia biashara zako mwenyewe angalau uwe na mtu mwaminifu na vile vile uwe unaonekana katika jambo lako angalau mara moja kwa siku kadhaa


Fact katika kila jambo fikiria vya mbeleni zaid usifikirie kesho tu maana kunakeshokutwa pia na namaanisha plan uwe nayo na muda mfupi na muda mrefu , plan ya muda mfupi itakusaidia kufanikisha plan yako ya muda mrefu.