Saturday, 18 April 2020

ITAFIKA WAKATI TANZANIA ITALIA SANA

Mpaka sasa watanzania wapo katika maombi ya siku tatu ambalo ni jambo jema maana kinaleta matumaini, JE MAOMBI TU YANATOSHA?

Waathirika wa COVID-19  wapo 147 hawajasema kati ya watu wangapi waliopimwa wala juhudi gani zinaendelea ili kujua ni watu wangapi wamepimwa na maambukizi mapya yapo ngapi,vifo vitano na waliopona 11.

Shughuli zinaendelea kama kawaida maana watanzania lazima tufanye kazi ndio tupate kula lakini ni mbinu gani serikali inatumia kuwanusuru watu wake na janga hili?

Serikali mpaka sasa imeshapima wananchi wake wangapi?

Kuna maabara ngapi mpaka sasa zinapima COVID-19?

Kutokujali, kutokuogopa,kutokuwa na hofu ya janga hili ni jambo jema lakini itafikia wakati TANZANIA ITALIA NA ISIJUE WAPI PAKUANZIA NA WAPI PAKUISHIA.

Sunday, 12 April 2020

WHO YASEMA COVID 19 YAWEZA RUDI KWA KASI ZAIDI KATIKA MIILI YA WALIOKUWA WAATHIRIKA YAANI WALIOPONA.

WHO yasema kuwa watu waliopona COVID-19 wako katika hatatari ya virus hao kupata nguvu zaidi na kurudi mwilini kwa kasi zaidi kuliko ilivyo kuwa mwanzo hii ni kutokana na nchi mbalimbali zinazotangaza idadi ya wangonjwa waliopona COVID-19

Korea ya kusini yatangaza kupima baadhi ya wahanga wa COVID-19 na kugundua kuwa bado wapo na maambukizi wakati hapo awali walikuwa wamepona kabisa.

Watanzania tunatakiwa tuchukulie hili jambo kwa umakini kabisa kama ni uchumi kuyumba utakuja yumba tu maana sehemu kubwa ya uchumi wetu tunategemea kuingiza vitu kutoka nchi zalizo endelea,watalii na hata bandari zetu kuingiza mizigo sasa kama nchi zingine zitaamua zote kufanya total lockdown sisi tusipo funga mipaka tutakuwa bado katika hali ngumu sana kiuchumi ukiongezea na umasikini wetu na madeni kama yote #NCHIISHAUZWAHII

Friday, 10 April 2020

IDADI YA VIFO KWA COVID-19 VYAFIKIA VITATU.

Idadi ya watu waliokufa kwa corona yafikia watu watatu Tanzania bara huku idadi ya waathirika ni 17 kwa Tanganyika na 7 Zanzibar which makes a total of 24 na waliokuwa caratin walikuwa 97 ila idadi ya watanzania waliopimwa jumla yao ni 1.8m ambao ni wale watu waliokuwa katika mahusiano na wagonjwa lakini ukwel kabisa idadi ya watanzania waliopimwa ni 0 na maambukizi mapya ni 0 sababu hakuna waliopimwa.

Monday, 6 April 2020

TANZANIA YAFANYA MZAHA KWA JANGA HILI LA COVID-19 (CORONA VIRUS).

Serikali ya Tanzania yaendelea kufanya mzaha kwa kutokuchukua hatua ambazo ni za hali ya juu katika kupambana na janga hili la corona virus.
Mpaka sasa hawajasitisha safari za ndege zinazotoka nje ya nchi wanaruhusu watu/watalii kutoka nchi zenye maambukizi kuingia nchini, haijakataza mikusanyiko kama makanisani,misikitini na cha zaidi sana wamefungua minada kifuatacho itakuwa ni kufungua shule na vyuo vyote.

Upimaji wa Corona virus hafifu yaani COVID-19 wao wanapima wasafiri tu ambao mpaka sasa wamefika 1.8m wakati Tanzania ina raia zaidi ya million 65, wanapima watu ambao waliokutana wa wagonjwa kama sio utani huo ni nini, mtu katokea airport amepanda usafir gani mpaka kwake amekutana na watu wa ngap kabla ya kufika kwake, kwa ujinga huu huu Tanzania itakuja kuwa na mlipo mkubwa sana katika siku zijazo maana tunachukulia janga hili kama utani tu.

Baadhi wa viongozi kupotosha watanzania eti Corona ni "mafua tu"  Mr Makonda amesema ivo,, kwani nan ameshawahi kuona mafua yanaua Corona inauwa na huu ni mwanzo tu kama hatutajihadhari mapema tutakufa kama kumbikumbi tena na huduma zetu za Afya hizi zilizo zorota, tutakuja kuwekwa kwenye kitabu cha historia kwamba kulikuwaga na nchi moja inayoitwa Tanzania iliyoangamizwa na virusi vya Corona ikapotea kabisa katika uso wa dunia.

Kuwa na namba ndogo wa wagonjwa wa Corona ni kutokana na upimaji hafifu wagonjwa wa Corona jumla yafikia 22 lakini kama watanzania tujiulize ni kweli kuwa wapo 22? na je kati ya watanzania 65m wameshapimwa wangapi mpaka sasa?, maambukizi mapya ni watu wangapi? na je hatua ambazo zimechukuliwa dhidi ya kupambana na janga hili zinatosheleza?

Ni wakati watanzania tunatakiwa kupaza sauti zetu kusema kipi kifanyike, sisi ndio wapiga kuna na sisi ndio wenye mamlka na kumpa dola ambae yupo madarakani na yeye lazima atusikilize sisi,