Thursday, 26 November 2020

MIKOPO,MISAADA NA UCHUMI WA KATI 2020.

Tanzania ni moja ya nchi iliyoingia katika uchumi wa kati Julai 2020, tukimaanisha kwamba kila mtanzania kwa mwaka anatengeneza kwanzia milion 2.3 mpaka 9. Tukiongelea ukweli uliopo mtaani ni kwamba hilo ni jambo ambalo si kweli bado kuna familia ambazo zinakula mlo mmoja kwa siku na watu wengine hawapati hata laki tano kwa mwaka licha ya kufikia 2.3m.

Ili kuendeleza shughuli za kimaendeleo Tanzania, serikali ya  Tanzania imekopa kutoka nje. BOT July 2019 ilisema deni la nje limefikia Dola Billion 21.6 sawa na Trillion 49Tsh na deni la ndani ni Trillion 15.5Tsh.
Kufikia January 2020 deni la nje limekuwa mpaka kufikia Trillion 54Tsh.

Janga la Corona limesababisha maafa katika nchi nyingi hasa kupunguzua kasi ya ukuwaji wa uchumi katika nchi nyingi, jambo ambalo limefanya Tanzania kukopa pesa na kupokea misaada mbali mbali kutoka nchi za nje, 
Mikopo na misaada Tanzania iliyopokea kwanzia Jangala Corona kuanza ni kama ifuatavyo.
1. Tanzania ilipokea euros million 27 kutoka EU ili kusaidia katika kupambana na janga la corona.
2. June 2020 Tanzania ilipokea hazina na misaada ambayo inathamani ya Dola million 14.3 kutoka International Monetary Fund.
3. September 2020 Tanzania ilikopa US Dola million 3.79 kutoka Worl Bank ili kusaidia katika matumiza ya maabara ya Taifa katika ugunduzi wa COVID-19 cases.
4. October 2020 Tanzania ilikopa Dola million 50.7 kutoka African Development Bank kwaajili ya kupambana dhidi ya corona.
5. Vile vile Tanzania ilipokea Dola million 500 kutoka World Bank kwaajili ya elimu ya kisasa.
6. Tanzania imeomba mkopo wa dola million 11 kutoka Global Fund(japo haiko wazi kama mkopo ulikubaliwa au la).

Sasa swali la kujiuliza ni kwamba, kama Siku tatu za maombi iliondoa Corona Tanzania pesa ambazo Tanzania iliokea September na October zilikuwa za nini na zilifanya shughuli gani wakati Corona ilishakwisha?

Mikopo ambayo Tanzania imepata kutoka nje inazidi kuongeza deni la nje, je serikali yetu ina jambo gani la kusema kuhusu hili.
Je bado deni la nje Tanzania inaweza kulimudu?
Je kodi za wananchi zinatumikaje mpaka kuwe na madeni makubwa namna hii?

Saturday, 15 August 2020

RUSHWA KUWA GUMZO KATIKA JESHI LA POLISI HUSUSANI KITENGO CHA USALAMA BARABARANI

Siku zote tunaamini kuwa jeshi la polisi linafanya kazi ya kulinda wananchi na mali zao, pindi wanapokwenda kinyume na hilo basi imani ya wananchi hupungua kwao.

Vitendo vya kupokea rushwa imeenea/kithiri katika jeshi la polisi sana, inafikipindi mpaka wananchi wanaomba msaada kwa mbunge wao maana wanakuwa wamechoshwa na vitendo hivyo. Katika jimbo moja Tanzania madereva boda boda imewalazimu kuomba msaada kwa mbunge wao ili wanusurike na vitendo vya rushwa kila wakati, nanukuu" mbunge sisi ni madereva bodaboda wa wilaya x(jina la wilaya nalihifadhi) tunaomba msaada wako maana tunanyanyaswa na polisi wa usalama barabarani mpaka tunahofia usalama wetu" 
1. Kukamatwa bila sababu ili wapate pesa.
2. Kupokea rushwa pindi wanapo pewa na kuomba waongezewe zaidi.

Magari ya kusafirisha abiria huwa abiria wanashuhudia ila watu huwaza wafike tu salama na kwa wakati katika safari zao lakini huwa ni kitendo kinacho kera abiria, japo madereva huwa na msemo kuwa "mkono mtupu haulabwi" ila ukweli ni kuwa wanakereka pia.

Utu ni muhimu kuliko pesa na usalama wa taifa ni jukumu la vyombo vya usalama(jeshi la polisi).


Sunday, 12 July 2020

Maisha Baada Ya Chuo

maisha baada chuo
Wasomi wengi sana especially ambao bado wapo mashuleni huwa wanafikiria kuwa watasoma mpaka shule ya msingi,sekondari,sekondari ya juu na chuo baada ya chuo wataajiriawa nakufanya kazi na kupokea mshahara alafu watajenga nyumba na kuwa na maisha mazuri. 
  • Mfumo wa elimu Tanzania unaanda wasomi waje kuwa waajiriwa na sio kujiajiri mwenyewe wala kujitegemea kwa kipato.
Sasa maisha baada ya chuo kwa wasomi wote huwa yanakuwa hivi
  • Kuna wale ambao watakuwa wanajitolea na hawalipwi kabisa
  • Kunaambao watakuwa wanajitolea na kulipwa kidogo, inafika wakati wanaona mda unakwenda na hakuna connection zozote zile mwishowe wanaacha
  • Kuna ambao watakwenda kufanya biashara mtaani(best of all) 
  • Kuna ambao watakuw wapo nyumbani tu hawana hili wala lile wanaangalia degree zao na kuchagua kazi maana wanaona hawana hadhi ya kufanya kazi ambazo sio za kisomi(worst kind) 
  • Kuna ambao watapata ajira katika sekta binafsi lakini wanaona kipato hakikidhi mahitaji
  • Kuna ambao watakuja kuwa wadangaji kwasababu ya ugumu wa maisha
  • Kuna ambao watakuwa wanapiga mishe za hapa na pale ili kupata hela za kuishi(mishen town) 
  • Kuna ambao watakuwa wakulima
  • Kuna ambao watakuwa wafugaji
  • Kuna ambao watakuwa inspiration talkers reality they got nothing 
  • Kuna ambao watakuwa wanabeti tu na kukwambia ramani hazisomi
  • Kuna ambao watakwenda kusoma masters
  • Kuna ambao watakuwa wanasiasa tu kwasababu wanatafuta pakutokea
  • Kuna ambao wataamua kuwekeza kwenye haya makampuni kama global alliance, forever living c, oriflame, na mengineyo mengi mpaka waje kusanuka kuwa huo mfumo hauwafaidishi wao ila walio tangulia kabla ndio wanaopata faida 
  • Kunaambao watakuwa wanajaribu kupata mafanikio the hard way(strugglers) ambao siku zote huwa watafanikiwa 
  • Kunaambao watakuwa wanajaribu hili na lile lakini huwa wanakata tamaa mapema na kushindwa kufikia lengo.
  • Huwa kuna aina nying sana za maisha na watu ambao watatokea baada ya masomo na baada ya kuanza maisha ya uraiani.
  1. News flash kwa wasomi wote kwamba the struggle is real especially to those ambao mnasoma bado muwe na mind set kwamba nikimaliza masomo sio lazima niajiriwe buni mbinj za kujipatia kipato ili uweze kuwa na maisha mazuri huko mbeleni, uwe umesoma ama haujasoma biashara au kazi yeyote ile hufanywa na watu wote hainaga kiwango cha elimu sema tofauti utaionyesha wewe ambae umesoma kwa kuifanya kazi yako kisomo na kwa uweledi wa juu kabisa onyesha elimu yako inakusaidi vipi kufanya biashara ama kazi uliyochagua kuifanya kwa quality ya juu kiasi gani ili iwe tofauti na ya watu wengine. 
  2. Think critically kama kwel wataka kutoka kimaisha jiwekee goals au target ya kwamba baada ya mwaka au miaka mingapi wataka kuwa na mafanikio kiasi gani, wataka kuwa na maisha ya aina gani ila sio kulala na kuwaza hela mwishowe uje kupata depression bure wakati haujishughulishi
  3. Kuwa na role model ambae utakuwa unalook up to him and desire to be economically better than him or at least reach where he is and more.
Siku zote huwa nasema if you want to be remembered with the future generations leave the greatest legacy behind you will never be forgotten.
BE THE LEGEND. 


Wednesday, 8 July 2020

UZEMBE wa MADAKTARI NA MANESI

uzembe wa madaktari na manesi katika kazi zao
Siku zote tunaamini madaktari sana, sasa uzembe mdogo wanaofanya madaktari na manesi unaweza ukapoteza maisha ya watu.Sisemi Vibaya ni bora Kuchukua tahadhari kuliko kuliko kujutia baadae.

Kuna mtu alikuwa anaumwa, kupelekwa hospital bila hata kujua historia ya mgonjwa vizuri wakamweka karantini,mtu anaumwa yupo serious kabisa lakini they overlooked kila kitu na kuhisi ni Corona, mgonjwa anahistoria ya kuumwa kifua, kama miaka mitatu sasa huwa anasumbuliwa na pneumonia, anatatizo la kutanuka, hakuwa na mafuwa wala kikohozi, joto la kawaida, alafu unampatia dawa za kutibu dalili za corona to be exact walikuwa wanampatia Azithromycin 250mg 2*2 kwa siku, mpaka akaanza kuzitapika yaan akimeza tu dawa anazirudisha that's how her body was protecting itself, overlooking details when it comes to health issues can be lethal.

Kuumua mtu mwenye pumu hauhitaji kumchoma sindano ya sumu, mtu akibanwa na kifua hawezi kupumua vizuri, unahis kama vile pumzi inataka kukata kabisa, ndio dawa ni muhimu maana inasaidia ila huwe safi ni muhimu sana maana ukikosa hewa safi mtiti ni ule ule, kumweka mtoto mdogo ambae amebanwa na kifua kwenye chumba ambacho kinanuka chlorine unategemea nini? Kinachoshangaza zaidi ni kuwa mtoto mdogo possibly <2 year suspected kuwa na corona wakati wazazi wake hawana, mtu mwenye pumu anaweza kuwa treated na dawa tofauti tofauti depends with how chronic ur illness is, no perfume,sprays,dust,stong scented oil and no cold, literally ur living a life of avoiding any strong smells and dust as much as you can so definitely no chlorine smell, i don't know who should be blamed for the death of that kid.

Mgonjwa ameletwa hospital yupo serious amelala kwa kitanda alafu hapati msaada wa haraka anaachwa OPD mpaka inafika wakati nduguzo wana mwinua mkono na kuuachia kuona kama bado yupo mzima, kwa hali kama hiyo alafu mbele za wagonjwa wengine kila mtu anapanic kivyake kila mtu anaona sasa ukisikia kifo kimekaribia ndio leo alafu bado we have to trust doctors and nurses.

Some doctors are always drunk na ndio amekuja kazini what can you say and ur sick you got no option just praying to God hoping he is not drunk enough to prescribe anything that comes to his mind.

Sometimes we have to question everything kujua kipi ni sahihi na kipi sio sahihi, don't trust blindly its lethal.


Thursday, 2 July 2020

JPM ANAFAA KWELI 2020 ?

jpm anafaa kwel 2020?Mtashangaa sana kwanini nasema kuwa 2015 uchaguzi ulifanyika na 2020 unafanyika tena.

Maana yangu kubwa ni kwamba utaona watu wengi sana wanasifia wanasiasa jambo ambalo sio baya ila watanzania tunatakiwa tuwaze sana ili tusije tukafanya mazoea kama tunavyofanya kila mwaka wa uchaguzi ukifika, hakuna sheria inayosema kwamba ni lazima kiongozi akae miaka kumi madarakani kama anafaa mpatieni dola aendeleze gurudumu lake la maendelea na kama hajatenda kama apaswavyo piga chini chagueni mwenye lengo jema la kuleta maendeleo.

1. Madiwani
..Jiulizeni sana diwani aliekuwepo madarakani amewatendea jambo gani la maendeleo katika kata zenu?
..diwani ametoa wazo gani katika kuleta maendeleo katika kata anayoitumikia?
..je diwani huyo mkimchagua tena atawaletea jambo gani katika kata yenu

Ni jukumu lenu kama wananchi kuchagua kiongozi bora ila mabadiliko na maendeleo ya patikane katika jamii yenu.

2. Wabunge
..mbunge wa wilaya yako amekuletea jambo gani la maendeleo kwa miaka mitano aliyokuwa madarakani?
Unfortunately mbunge wa wilaya niliyopo mimi yeye alichokifanya ndani ya miaka mitano ni kununua gari lake tu, hakai ofisini wala hoja zake zote alizotoa sidhani kama amezitimiza.
..je mbunge wako alitimiza ahadi zake alizotoa wakati wa kampeni miaka mitano iliyopita?
..je atafaa tena kuwepo madara kani?

3.Raisi
..raisi aliepo madarakani ametimiza hoja zake alizoto/ahidi wananchi?
..je ameleta maendeleo gani katika miaka mitano aliekuwepo madarakani?
.. Changamoto ya umasikini kwa mtu mmoja mmoja ameitatua vipi? Tena angalieni sana watu ambao wapo mijini na vijijini ambao wapo kwenye mzunguko wa umasikini usiangalie wale watu ambao ni matajiri ndio mtajua ninachokimaanisha ninauhakika kuna yule mtu apo mtaani kwako ambae unamuonea hafi huruma maana hata chakula cha siku hajui atakipataje na hajui hata kama kesho ataamka, anakula mlo mmoja siku nzima, nguo ndo bas tena kesho ikifika ni majaaliwa mateso yale yale ya jana tena bora na jana yake, masikini wamesaidika vip?
..Aliyotenda yanaonekana na ambayo hayajatendeka yanaonekana je ametenda kwa asilimia ngapi?
..kutokana na asilimia ulizo mpa je anafaa kuwa madarakani tena?

Watanzania tuko na tatizo moja tu yaan utazani tuanaugonjwa wa kusahau, msikubali kuhongwa vijihela vya mboga ya kula jioni tu alafu ukajitia hasara na kupoteza miaka mitano ambayo ungepata mafanikio na kupata pesa za kutumia miaka yote hiyo mitano na kwa siku nzima, tusikubali kuchagua mtu ambae hatatuletea badiliko lolote katika miaka mi tano ambayo unampa akaipoteza bure, tusikubali kugongwa kama mpira wa kona na kuingia nyavuni wakati ungekuwa unafutahia kuwa uwanjani unawapa wachezaji changamoto.

Tuondoe dhana kuwa kiongozi ni yule anaetoka chama fulani, hapana, kiongozi bora anatoka chama chochote, kiongozi mwenye sera na uchu wa maendeleo katika wilaya, kata, mtaa, na hata nchi yake huyo ndio kiongozi anaetufaa, kiongozi ambae anakuwa sauti ya kwel ya wananchi ndio anaefaa, kiongozi ambae akikaa hata katika familia yake anatamani na anakuja na wazo jipya ya kuiimarisha familia yake kiuchumi ndio anaefaa, kiongozi ambae anaona baada ya miaka mitano jamii yake ataibadilisha katika nyanja mbali mbali ndio anaefaa.

Mwaka wa uchaguzi tufanye maamuzi sahihi bila kushurutisha na nguvu ya vijihela vya chini ya kapeti wala nyuma ya pazia, tufanye maamuzi sahihi kwaajili ya baadae sio kwaajili ya sasa tu ata wajukuu zenu waje kuwakumbuka kwa kufanya jambo zuri huko baadae.

If you want to be a legend leave a great legacy behind no one will forget you forever.


Saturday, 18 April 2020

ITAFIKA WAKATI TANZANIA ITALIA SANA

Mpaka sasa watanzania wapo katika maombi ya siku tatu ambalo ni jambo jema maana kinaleta matumaini, JE MAOMBI TU YANATOSHA?

Waathirika wa COVID-19  wapo 147 hawajasema kati ya watu wangapi waliopimwa wala juhudi gani zinaendelea ili kujua ni watu wangapi wamepimwa na maambukizi mapya yapo ngapi,vifo vitano na waliopona 11.

Shughuli zinaendelea kama kawaida maana watanzania lazima tufanye kazi ndio tupate kula lakini ni mbinu gani serikali inatumia kuwanusuru watu wake na janga hili?

Serikali mpaka sasa imeshapima wananchi wake wangapi?

Kuna maabara ngapi mpaka sasa zinapima COVID-19?

Kutokujali, kutokuogopa,kutokuwa na hofu ya janga hili ni jambo jema lakini itafikia wakati TANZANIA ITALIA NA ISIJUE WAPI PAKUANZIA NA WAPI PAKUISHIA.

Sunday, 12 April 2020

WHO YASEMA COVID 19 YAWEZA RUDI KWA KASI ZAIDI KATIKA MIILI YA WALIOKUWA WAATHIRIKA YAANI WALIOPONA.

WHO yasema kuwa watu waliopona COVID-19 wako katika hatatari ya virus hao kupata nguvu zaidi na kurudi mwilini kwa kasi zaidi kuliko ilivyo kuwa mwanzo hii ni kutokana na nchi mbalimbali zinazotangaza idadi ya wangonjwa waliopona COVID-19

Korea ya kusini yatangaza kupima baadhi ya wahanga wa COVID-19 na kugundua kuwa bado wapo na maambukizi wakati hapo awali walikuwa wamepona kabisa.

Watanzania tunatakiwa tuchukulie hili jambo kwa umakini kabisa kama ni uchumi kuyumba utakuja yumba tu maana sehemu kubwa ya uchumi wetu tunategemea kuingiza vitu kutoka nchi zalizo endelea,watalii na hata bandari zetu kuingiza mizigo sasa kama nchi zingine zitaamua zote kufanya total lockdown sisi tusipo funga mipaka tutakuwa bado katika hali ngumu sana kiuchumi ukiongezea na umasikini wetu na madeni kama yote #NCHIISHAUZWAHII

Friday, 10 April 2020

IDADI YA VIFO KWA COVID-19 VYAFIKIA VITATU.

Idadi ya watu waliokufa kwa corona yafikia watu watatu Tanzania bara huku idadi ya waathirika ni 17 kwa Tanganyika na 7 Zanzibar which makes a total of 24 na waliokuwa caratin walikuwa 97 ila idadi ya watanzania waliopimwa jumla yao ni 1.8m ambao ni wale watu waliokuwa katika mahusiano na wagonjwa lakini ukwel kabisa idadi ya watanzania waliopimwa ni 0 na maambukizi mapya ni 0 sababu hakuna waliopimwa.

Monday, 6 April 2020

TANZANIA YAFANYA MZAHA KWA JANGA HILI LA COVID-19 (CORONA VIRUS).

Serikali ya Tanzania yaendelea kufanya mzaha kwa kutokuchukua hatua ambazo ni za hali ya juu katika kupambana na janga hili la corona virus.
Mpaka sasa hawajasitisha safari za ndege zinazotoka nje ya nchi wanaruhusu watu/watalii kutoka nchi zenye maambukizi kuingia nchini, haijakataza mikusanyiko kama makanisani,misikitini na cha zaidi sana wamefungua minada kifuatacho itakuwa ni kufungua shule na vyuo vyote.

Upimaji wa Corona virus hafifu yaani COVID-19 wao wanapima wasafiri tu ambao mpaka sasa wamefika 1.8m wakati Tanzania ina raia zaidi ya million 65, wanapima watu ambao waliokutana wa wagonjwa kama sio utani huo ni nini, mtu katokea airport amepanda usafir gani mpaka kwake amekutana na watu wa ngap kabla ya kufika kwake, kwa ujinga huu huu Tanzania itakuja kuwa na mlipo mkubwa sana katika siku zijazo maana tunachukulia janga hili kama utani tu.

Baadhi wa viongozi kupotosha watanzania eti Corona ni "mafua tu"  Mr Makonda amesema ivo,, kwani nan ameshawahi kuona mafua yanaua Corona inauwa na huu ni mwanzo tu kama hatutajihadhari mapema tutakufa kama kumbikumbi tena na huduma zetu za Afya hizi zilizo zorota, tutakuja kuwekwa kwenye kitabu cha historia kwamba kulikuwaga na nchi moja inayoitwa Tanzania iliyoangamizwa na virusi vya Corona ikapotea kabisa katika uso wa dunia.

Kuwa na namba ndogo wa wagonjwa wa Corona ni kutokana na upimaji hafifu wagonjwa wa Corona jumla yafikia 22 lakini kama watanzania tujiulize ni kweli kuwa wapo 22? na je kati ya watanzania 65m wameshapimwa wangapi mpaka sasa?, maambukizi mapya ni watu wangapi? na je hatua ambazo zimechukuliwa dhidi ya kupambana na janga hili zinatosheleza?

Ni wakati watanzania tunatakiwa kupaza sauti zetu kusema kipi kifanyike, sisi ndio wapiga kuna na sisi ndio wenye mamlka na kumpa dola ambae yupo madarakani na yeye lazima atusikilize sisi,


Thursday, 6 February 2020

KUWA NA KADI YA UANACHAMA WA CCM NI SIFA MOJAWAPO/TAJWA YA KUGOMBEA NAFASI YA KAZI ZA WATENDAJI WA MITAA ZILIZOTANGAZWA FEBRUARY 2020.,

Serikali ya Tanzania inapoeleke kitakuwa ni chama kimoja, demokrasia ya kweli na haki za wapinzani za zidi kupote.  Naamini kwamba Tanzania haitakuwa na mabadiliko hadi pale ambapo chama kilichopo madarakani kukubaliana na mfumo wa vyama vingi na demokrasia ya kweli ili kuleta mabadiliko na maendeleo katika nchi ya Tanzania. 
Sifa mojawapo ambayo imetajwa kwa kugombea ambao wanatakiwa kugombea nafasi za watendaji wa mitaa ambayo imetangazwa na serikali ni kuwa na kadi ya uanachama wa chama cha CCM. Leo mapema asubuhi nikiwa katika mahojiano na mwenyenia ya kugombea amesema kwamba ameulizia sifa za kugombea na moja wapo nikuwa lazima awe na kadi ya uanachama wa chama cha CCM. 
Tunasema Tanzania ni nchi yenye mfumo wa vyama vingi ila ukweli ni kwamba chama kinacho tawala ni kimoja na kinazidi kupoteza maana ya mfumo wa vyama vingi kwa kuwakandamiza wanasiasa wanaotokea kwenye vyama vya upinzani na kuwanyima nafasi ya kuleta maendeleo katika nchi ya Tanzania. 
2020 wananchi wote tunatakiwa kuangalia sera ambazo zitasaidia kueta maendeleo katika nchi yetu na si kuchagua chama kama tunavyofanya kwa mazoea ni wakati ambao tunatakiwa kujua kuwa kama kweli miaka 43 ya uongozi wa chama cha mapinduzi CCM mpaka sasa shida ni zilezile tena ndio zinaongezeka kila siku maradufu bora ya jana kwanini tunaendelea kulea siasa ambazo hazina tija nchini mfano marekani wakishida chama cha Republican msimu ujao kinashinda chama kingine ndio maana ata siasa zao zipo viziri maana wananchi wake wanachagua sera na sio chama kama watanzania tunavyofanya. 
Kwa wazalendo wote ni vizuri tukapenda nchi yetu na kuchagua sera za maana ambazo zitatuletea mabadiliko chanya nchini. 


Sunday, 19 January 2020

SIASA MPAKA KWENYE MAKAMPUNI ZA MAWASILIANO, VITAMBULISHO VYA NIDA YAWA GUMZO.

Watanzania wanaendeshwa sana na siasa zisizo kuwa na mipango, wenye siasa yao wameona njia pekee ya kufanya watanzania wajiandikishe ili wapate vitambulisho ni kutoa tamko kuwa kila mtanzania anatakiwa asajili lain yake kwa alama za vidole, mnatishia kufungia watu lain zao bila kusahau hata TCRA haina mamlaka ya kufungia watu mawasiliano ila makapuni ya mawasiliano kama Tigo, Vodacom, Airtell, Halotel,  Ttcl...  Ndio yenye uwezo wa kufanya hivyo, pia hiyo inahusu mwenye kampuni yake na wateja wake haihusu wanasiasa hata kidogo. 

1. Uzembe ambo umefanywa na NIDA ndio umesababisha watu mpaka sasa wengine hawana namba za vitambulisho na hata vitambulisho kabisa tena bila haya ukienda kwenye ofisi zao wanakwambia eti namba yako bado endelea kusubiri inakuwaje mnawapa watanzania dead line lakini mnasahau watu wa kupewa dead line ni kina nani,  wanasiasa tumieni akili na sio ndimi zenu. 
2. Makampuni ya mawasiliano hawawezi kupata faida katika biashara zao, makampuni ya simcard zote zitapata hasara maana wanapunguza wateja wao tena kisa siasa mbovu za Tanzania, sasa serikali itailipa makapuni ya mawasiliano ama la? maana mnazisababishia hasara na je mtategemea kulipwa kodi maana mnawapatia hasara za bure. 
3. Makampuni ya mawasiliano mnatakiwa mdai haki yenu, najua mtakuwa na policy zenu na sheria zenu ambazo zinaonyesha nani anauwezo wa kufanya maamuzi katika makamupuni yenu najua hamna sehemu ambayo imeandika mwanasiasa ama raisi wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania. 
4. Watanzania wote mnatakiwa mdai haki yenu ya mawasiliano, mawasiliano ni haki ya kila mtanzania pia hamna serikali bila wananchi, wananchi ndio serikali yenyewe maana nchi bila kodi za wananchi haiwezi kujiendesha pia usisahau katika kulipa kodi mpaka kodi ya mawasiliano unayotumia unalipia. Watanzania tunatakiwa tuache uwoga usio kuwa na maana na kuzidi kuwa watumwa huru katika nchi yetu ambayo ni huru. 
Sasa watanzania dhamana ya mawasiliano yetu ipo katika mikono yetu wenyewe,  ni chaguo letu kuendelea kupelekwa na wanasiasa kama ng'ombe wanaokwenda kunywa maji yaani kukubali kuburutwa na siasa mbovu za Tanzania ama kuamua kudai haki zetu za msingi na kupata kinachostaili katika maisha yetu.